Mkuu wa Udhibiti wa Airtel Africa na Mwenyekiti wa Kundi la Sera Afrika la GSMA, Bw. Daddy Mukadi, amezitaka serikali za Afrika kuitambua sekta ya mawasiliano ya simu kama nguzo kuu ya uchumi, huku akipendekeza mageuzi mawili muhimu ya kodi yatakayochochea kwa kasi ujumuishaji wa kidijitali barani.

