Back to top

News

Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mhe.Mama Mariam Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kutambua na kuthamini mchango wa Wanawake na kuwashirikisha katika ngazi ya maamuzi na kuendeleza maendeleo nchini.