Watu 46 wameathirika baada ya kuvuta hewa yenye Sumu kutoka kiwanda cha kutengeneza Sabuni cha ROYAL kilichopo Mabibo external Jijini Dar Es Salaam.
Meneja Operesheni wa kiwanda hicho Bw. Ntuta Shalanda amesema hewa hiyo imevuja kutokana na hitilafu kwenye mtambo wa kuchuja tindikali na tayari wamedhibiti tatizo na wamewachukua waathirika wote na kuwapeleka hospitali kwa matibabu kwa garama zao.
Mkuu wa wilaya ya Ubungo Bw. Kisare Makori amefika eneo la tukio na kuagiza wananchi walioathrika na tukio hilo wafidiwe na mazungumzo yaanze mara moja kuna namna yakuhamisha wanaoishi karibu na kiwanda ili kuepusha madhara zaidi.
Wananchi wa maeneo jirani wamekubali ushauri wa mkuu wa wilaya na kutaka uhakiki wa athari za mazingira ufanyike kujiridhisha kama kinafuata sheria na taratibu.