Watu wawili wamefariki dunia katika nyakati tofauti mkoani geita akiwemo Joseph Maneno mkazi wa kijiji cha Senga akidaiwa kujinyonga kwa kutumia kipande cha nyavu ya kuvulia samaki ndani ya ofisi ya mtendaji wa kijiji cha Kagu a Mkoani Geita alipokuwa akishikiliwa kwa tuhuma za wizi wa fedha na simu ya mkononi.
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Mponjoli Lotson anasema jeshi hilo linaendelea na uchunguzi wa kifo cha mtuhumiwa huyo kutokana na utata ulioibuka huku akiwataka watendaji wa vijiji na kata kufuata sheria katika ukamataji na usalama wa watuhumiwa.
Kamanda Mponjoli anasema tukio la pili limehusisha kifo cha Salago George kilichosababishwa na ajali ya gari ndogo mbili kugongana uso kwa uso katika eneo la Mpomvu wakiwa katika mwendo kasi na kusababisha majeruhi wanne ambao wanaendelea kupata matibabu katika hosipitali ya mkoa wa Geita na Bugando.