Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Soka Tanzania (FAT) kwa sasa ikitambulika TFF, Alhaj Muhidin Ndolanga amefariki dunia jioni hii katika hospitali ya TMJ Dar es Salaam.
.
Rais wa TFF Wallace Karia ametoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki na wanafamilia wa mpira walioguswa na msiba huo.
.
Karia amesema Marehemu Ndolanga wakati wa uhai wake alikuwa anapenda kuona mpira wa miguu unapiga hatua kwenda mbele.