Wananchi wa kijiji cha Mbuluma wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamemuua kwa mchoma moto Amosi Kapufi miaka 22 mkazi wa kijiji cha Myunga Kwa kile kilichodaiwa kumchoma kisu mtoto wa dada yake aliyefahamika kwa jina la Catherin Kakusu na kufariki dunia papo hapo.
Vilio na huzuni kubwa imetanda kwa wakazi wa kijiji cha Myunga baada ya kumpoteza kijana wao Amos Kapufi baada ya kupigwa kisha kuchomwa moto na wananchi baada ya kudaiwa kusababisha kifo cha binti Catherin Kakusu mkazi wa Mbuluma kutokana na wivu wa kimapenzi .
Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura amethibitisha kutokea tukio hilo na kuwasihi wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi.
Hata hivyo inadawa kuwa kijana huyo alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na binti huyo na baada ya kutofautiana aliamua kuchoma na kisu katika sehemu za tumbo na kifuani na kusababisha kifo cha binti huyo.