Jeshi la polisi mkoani Mwanza linamsaka Adam Athuman mkazi wa eneo la Nyamadoke wilayani Ilemela kwa tuhuma za kumpiga na kumsababishia kifo mtoto wake Athuman Adam mwenye umri wa miaka 10 mwanafunzi wa shule msingi Nyamadoke.
Kamanda polisi mkoa wa Mwanza Muliro Jumanne Muliro anathibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa jeshia hilo linamtafuta mhusika ili aje kujibu tuhuma zake.
Tukio hilo linatokea wakati maadhimisho ya siku 16 ya za kupinga ukatili yakiendelea duniani kote ambapo viongozi wa serikali ya mtaa alipokuwa akiishia marehemu huyo wamekemea ukatili huo na kuziomba mamlaka husika kuchukua hatua.
Majirani hao wamesema mara nyingi inaaminika kuwa mikononi mwa wazazi ni sehemu salama kwa watoto, lakini tukio hili linalodaiwa kufanywa na baba mzazi wa mtoto linamewasikitisha na kuwafanya wafikirie tofauti.