Back to top

Baba na mtoto washambuliwa kwa mapanga na mishale Tarime.

05 January 2020
Share

Watu wawili wa familia moja baba na mtoto wake wakazi wa kijiji cha Kenyamusabi mkoa wa Mara  wamejeruhiwa kwa  kwa kuchomwa na mkuki na kukatwa katwa na mapanga  kutokana na migogoro ya ardhi  kati yao na familia ya Rhobi Daniel ambayo imetokomea kusikojulikana baada ya tukio hilo.

Akielezea tukio hilo Mwenyekiti wa kijiji   hicho Mwita Raphael ametaja majeruhi hao kuwa ni John Joel baba mzazi na mwingine ni Hula John mtoto wa Joel ambaye yeye amechomwa mkuki ubavuni  huku baba akijeruhiwa kwa kukatwa na panga sehemu mbalimbali za mwili wake .