Vitendo vya biashara ya magendo ya Kahawa vimeshamiri wilayani Mbinga mkoani Ruvuma ambapo serikali wilayani humo imekamata shehena ya Kahawa ya magendo ikiwa katika mifuko 600 ya sandarusi katika ghala bubu linadaiwa kumilikiwa na Bw. Joackim Kohelo.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga Bw. Juma Mnwele amesema Kahawa hiyo imekamatwa baada ya msako kuwabaini watu wanaonunua Kahawa kwa watui binafsi badala ya kupitia kwenye vyama vya ushirika.
Kwa upande wake mtuhumiwa Joackim Kohelo amesema kuwa hakununua kahawa hiyo bali amelima kwa kushirikiana na ndugu zake.