Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga Dkt. Halfani Haule amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Sumbawanga Jacobu Mtalitinya kuhakikisha anawahamishia kwenye hosteli wanafunzi wote wa kike wanaotembea umbali wa zaidi km 20 kutoka Nambogo hadi Moro wakati wakienda Shule ya Sekondari Kalangasa kwa lengo la kuwaepusha na vishawishi ambavyo vinaweza kusababisha kukatisha masomo yao ikiwemo kupata ujauzito.