Back to top

Dkt.Shein amuapisha Mwenyekiti mpya wa Tume ya Uchaguzi - ZEC.

22 June 2018
Share

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amemuapisha Mwenyekiti mpya wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar Mhe. Hamid Mahmoud huku Mwenyekiti huyo akiahidi kufuata katiba na sheria.

Hafla hiyo ya kuapishwa Mwenyekiti ilifanyika Ikulu na kuhudhuriwa na viongzoi wa juu wa Serikali akiwemo Makamu wa pili Balozi Seif Ali idi, Spika wa Baraza Mhe.Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar  Omar Othman Amkungu, wakuu wa vikosi vya SMZ na watendaji wengine.

Mbali ya Mwenyekiti mpya wa ZEC, Dkt. Shein pia aliwaapisha Makamishna wapya wa tume hiyo ambapo na Mabruki Jabu Makame na Fateh Saad Mgeni kutoka CCM, Makame Pandu wa CUF, Dkt. Kombo Khamis Hassan wa NLD,na wengine na jaji wa Mahakama kuu Khamis Ramadhan Shaabn na Bi.Jokha Khamis Makame ambaye alikuwa ni afisa mdhamni wa afisi ya Rais Pemba.

Mwenyekiti mpya wa tume hiyo Mhe.Hamid Mahmud ambaye pia ni Makamu Mwenyekti wa tume ya uchagzu ya taifa - NEC amesema atahakikisha anafanyaa kazi zake kwa uadilifu kwa kufuata katiba na sheria na kanuni bila upendeleo.