Back to top

EAC yakanusha Mhe.Mkapa kukosa ushirikiano utatuzi mgogoro wa Burundi.

08 February 2019
Share

Naibu  Katibu mkuu wa  Jumuiya ya  Afrika  mashariki  (EAC)  amekanusha  taarifa zinazoenea  kwenye  mitandao  ya Kijamii  zikidai  kuwa  Msuluhishi  wa  mgogoro  wa  Burundi  Rais  Mstaafu  wa  Tanzania  Benjamin  Mkapa  amelalamika  kukosa  ushirikiano  wakati  alipokuwa  anafanya kazi  ya  usuluhishi  wa  mgogoro huo
  
Akizungumzia  taarifa  hizo  za mitandao  ya kijamii  Jijini   Arusha  Naibu  katibu  mkuu  wa  Jumuiya hiyo Mhandishi  Steven  Mlote  amesema ni  za  uzushi  na zinapaswa  kupuuzwa  kwani  zinatolewa  na  watu  wasioitakia  mema  Jumuiya  hiyo
  
Aidha Mhandisi  Mlote  amefafanua  kuwa  Mhe.Mkapa  alishamaliza  kazi  yake  na  kuikabidhi  kwa  wakuu  wa  nchi   wanachama  ambao  licha  ya  kumshukuru  kwa  kazi  nzuri  aliyoifanya  na  pia  walipongeza  ushirikiano  mkubwa  uliotolewa  na  sekretarieti  ya  Jumuiya  hiyo  wakati  wote  wa  mazungumzo
  
Bw.Mlote  amesema  kimsingi  Jumuiya  ya  Afrika  mashariki haina  tatizo  lolote  na  aliyekuwa  msuluhishi  wa  Mgogoro  huo   na  kwamba  kwa  sasa  inaendelea  kutekeleza  maelekezo  ya  wakuu  wan chi  wanachama   yakiwemo  ya  kuongeza  kasi  ya  kusimamia  miradi  mbalimbali  ya  kuwaunganisha  wananchi   wa  nchi  wanachama   kiuchumi  kijamii  na  kisiasa  

Taarifa  zinazoenea  kwenya baadhi  ya mitandao  ya  kijamii  zinaeleza  kuwa aliyekuwa  msuluhishi wa Mgogoro  wa  Burundi  amelalamika  kuwa  alikosa  ushirikiano wa watendaji  wa Jumuiya   hiyo   wakati  wa  mazungumzo  hayo  .