Back to top

Familia zilizotelekezwa na wanaume Mwanza zasaidiwa chakula.

14 June 2020
Share

Vitendo vya wanaume kutelekeza wanawake na watoto vinatajwa kuongezeka katika wilaya Misungwi mkoani Mwanza na kusababisha kaya hizo kuishi maisha ya dhiki ambapo Shirika la Kivulini limetoa msaada kilo 1000 za mchele kwa kaya 20 ambazo zimeathirika na ukatili  huo wa kijinsia.


Vitendo hivyo vya wanaume kutelekeza familia zao vinaelezwa kuwa na  athari kubwa ikiwemo upatikanaji wa chakula pamoja na mahitaji mengine muhimu ya kijamii.