Back to top

Huduma za afya zaathiriwa na kukosekana kwa umeme Lupembe

14 December 2018
Share

Kituo cha afya Lupembe wilayani Njombe kinakabiliwa na changamoto ya kukosa umeme kwa takribani mwezi mmoja sasa kutokana na Transfoma iliyokuwepo  kuharibika  na kusababisha baadhi ya huduma muhimu katika kituo hicho zikiwemo za vipimo na  upasuaji  kushindwa kutolewa.

Kaimu mganga mfawidhi wa kituo cha afyaLupembe  Dkt. Eliud Kibona ameeleza kuwa kutokana na kukosekana kwa nishati ya umeme wanalazimika kutumia  mtambo wa mafuta (jenereta) ambao huwashwa kwa muda mfupi na kwamba baadhi ya huduma muhimu zinashindwa kutolewa kituoni hapo .

Akizungumza kwa niaba ya meneja wa shirika la umeme  TANESCO mkoa wa Njombe afisa mahusiano wa shirika hilo Bi.Veronica Magoti amesema tatizo hilo linatambuliwa na linatafutiwa ufumbuzi ndani ya muda mfupi.