Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewaonya viongozi wa kisiasa nchini kuacha kufanya siasa za ushari kwa kuzungumza maneno ya ukali wanapoeleza sera zao kwa watanzania.
IGP Sirro amesema hayo katika mahojiano na kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na ITV kila Jumatatu saa tatu kamili Usiku.
Katika hatua nyingine IGP Sirro amewashauri vijana kutojiinga katika masuala ambayo yanafanywa kwa maslahi ya watu wachache kuelekea Uchaguzi Mkuu.