Back to top

Jumuiya ya Ulaya yapiga kura kuiwekea vikwazo Hungary.

12 September 2018
Share

Jumuiya ya Ulaya imepiga kura kuiwekea vikwazo nchi ya Hungary kwa kile kinachoelezwa nchi hiyo kukiuka misingi ya demokrasia inayofanywa na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Victor Orban ambaye hivi  karibuni aliweka vikwazo dhidi ya wahamiaji wanaoingia nchini humo, kubana uhuru wa habari na kuweka sheria mpya za uendeshaji wa taasisi za elimu ya juu.