Back to top

Madaktari bingwa Arusha watoa matibabu ya bure kwa wanyamakazi.

19 September 2018
Share

Jopo la watalaam wa mifugo na madaktari bingwa wa wanyama  mkoani Arusha wameanza kutoa matibabu ya bure kwa wanyamakazi aina ya punda  kihongo  wenye  vidonda  na majeraha makubwa kwenye miili yao inayotokana na kubebeshwa mizigo mizito bila matibabu huku wafugaji wakisema hawaoni sababu ya kumtibu mnyama huyo kwani si kwa matumizi ya kitoweo.

Watalaam  hao wa mifugo  wanasema wameamuwa kutoa huduma ya matibabu ya bure baada ya kuguswa na mateso wanayoyapata wanyama hao ambao hivi sasa wanatishio la kutoweka baada ya kukithiri kwa wizi wa wanyama hao huku baadhi ya waliowahi kupatiwa elimu ya ufugaji bora wa punda wakieleza walivyobadilika baada ya elimu hiyo.

Watetezi wa haki za  wanyama wanasema wanaishukuru serikali kwa kuunga mkono juhudi zao katika utetezi wa wanyama kazi ambao utumikishwa bila kupatiwa haki ya kutibiwa.