Back to top

Mafuta ya Kula yakamatwa yakisafirishwa kupelekwa nje ya nchi Zanzibar

24 May 2018
Share

Wakala wa Chakula na Dawa Zanzibar  wamefanikwa kukamata Shehena ya  Magaloni 740 ya mafuta ya Kula ambayo yalikuwa yasafirishwe kwenda nje ya Zanzibar baada ya kubadilishwa nembo ya awali na kuwekwa nembo ya Oki.

Wakala wa Chakula na Dawa Zanzibar-ZFDA-imefanikiwa kunasa shehena ya  magaloni 740 ya mafuta ya kula yaliyokuwa yasafirishwe nje ya Zanzibar   baada ya kubadilshwa nembo yake halisi na kuwekwa nembo ya Oki,magaloni hayo 740 yalikuwa yamehifadhiwa ndani ya tawi la CCM makadara Zanzibar.

Akizumgumza na vyombo vya habari katika eneo la operesheni hiyo makadara mjini Unguja ambapo magaloni hayo yalikuwa  yakigeuzwa nembo za asili ndani ya tawi hilo la CCM Makadara  kaimu mkurugenzi mtendaji  wa wakala huo Dkt. Khamis Ali Omar amesema  walipata taarifa  na kuvamia eneo hilo wakati wa usiku na kukuta shehena hiyo huku mmiliki huyo akitoweka  na anatafutwa ,mtendaji huyo amethibitisha kuwa mafuta ijayo yenye nembo ya Turkey yatoka Indonesia .

Kuonekana kwa mafuta hayo ndani ya tawi la CCM ilizua mjadala mkubwa  na hofu ya tawi hilo kuhusika hata hivyo akiongea kwa simu naibu katibu mkuu CCM Dkt. Abdulah Juma Mabodi amekanusha CCM kuhusika kauli ambayo iliungwa mkono na katibu wa  CCM jimbo la Malindi  Salum Juma Ali aliyefika kwenye tukio hilo,huku mwakilishi wa kampuni hiyo ya Oki  Zanzibar  Salum Humud wa Sub Sahara amesema ni mtindo ambao lazima upigwe vita na serikali. 

Wakti zoezi la kutaka kuyaondosha mafuta  hayo  likianza mmoja ya mtu anayetuhumiwa kuhusika na  zoezi hilo  aliibuka na  kudai  yeye hajui chochote   n awalikuwawnatumiaeneo hulo kuhifadhi ndai ya tawi  la ccm.