Makamu wa Rais mh. Samia Suluhu Hassani amepiga marufuku tabia ya halmashauri ya wilaya ya Moshi kuendelea kuwatoza wakulima wa mpunga ushuru wa mazao mashambani msimu wa mavuno.
Makamu wa Rais ameyasema hayo baada ya kupokea malalamiko kwa wakulima wa mpunga kata ya Mabogini skimu ya umwagiliaji Lower Moshi kutozwa kodi mashambani kabla ya kutoa mazao shambani.