Mbwa wanaodhaniwa kuwa na ugonjwa wa kichaa cha mbwa wamekuwa tishio katika wilaya ya Gairo mkoani Morogoro baada kumg’ata mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitatu na kufariki kisha kujeruhi watu wengine sita kwa nyakati tofauti hali iliyo lilazimu baraza la madiwani wa halmashauri hiyo kutoa siku 10 kwa wataalamu wa afya ya wanyama kudhibiti wanyama hao kabla hawajasababisha madhara makubwa.
.
Kufuatia hali hiyo Afisa mifugo na uvuvi wa wilaya ya Gairo Dr.Godbless Luhunga amesema watapunguza idadi ya kuzaliana kwa mbwa hao.