Back to top

Mfanyabiashara Mo Dewji apatikana, polisi yaonya wanaoharibu uchunguzi

20 October 2018
Share

Jeshi la Polisi Tanzania limewaonya watu wanaoingilia kazi za polisi katika upelelezi wa makosa mbalimbali kwa  kulielekeza namna ya kufanya shughuli zake kwa ukamilifu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi SIMON SIRRO ametoa onyo hilo alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya kumpata mfanyabiashara maarufu nchini MOHAMMED  DEWJI au 'MO', aliyekuwa ametekwa katika hoteli ya Collesium jijini Dar es Salaam Oktoba 11,2018 saa kumi na moja alfajiri alikokwenda kwa ajili ya mazoezi ya viungo.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Sirro akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kufanikiwa kumpata mfanyabiashara Mohammed Dewji aliyekua katekwa Oktoba 11, 2018.
Hili ndio gari ambalo limetumika kumteka mfanyabashara maarufu nchini Tanzania Mohammed Dewji'MO', aliyetekwa katika hoteli ya Collesium jijini Dar es Salaam Oktoba 11,2018.
Huyu ndiye Mohammed Dewji ambaye alitekwa na watu wasiojulikana Oktoba 11,2018 alipokuwa akielekea katika hoteli ya Collesium jijini Dar es Salaam kufanya mazoezi ya viungo.

Leo Oktoba 20, Mo Dewji alipatikana katika eneo la Gymkana Dar es Salaam akiwa katelekezwa na wasiojulikana, Picha hiyo ni kabla ya kutekwa.

Kamanda SIRRO amesema yeyote atakefanya hivyo atachukuliwa hatua stahiki bila kujali kama anafanya kwa faida yake au aliyemtuma.

Amewataka watu wenye mapenzi mema na taifa, wandelee kutoa ushirikiano katika upelelezi wa tukio hilo unaoendelea kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola hadi wahusika watakapokamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Akielezea mazingira ya kuachiwa kwa mfanyabiashara huyo leo saa kumi na moja alfajiri katika viwanja vya Gymkana, Kamanda SIRRO amesema polisi walikamata bunduki moja aina ya AK-47, bastola tatu pamoja na risasi kadhaa.

Baada ya kulibaini gari lililo tumika kumteka "Mo' Polisi walikuta bunduki moja aina ya AK-47, bastola tatu pamoja na risasi kadhaa.
Hili ndio gari lililotelekezwa na watekaji katika eneo la Gymkana Jijini Dar es Salaam Oktoba 20,2018