Back to top

Milipuko na milio ya risasi yasikika Nairobi,Kenya.

15 January 2019
Share

 

Milipuko na milio ya risasi imesikika katika eneo la 14 Riverside, Nairobi ilipo hoteli ya kifahari ya DusitD2 .

Msemaji wa kundi la kigaidi la al-Shabab ameliambia shirika la habari la BBC kuwa kundi hilo ndiyo limehusika katika tukio hilo.

Wataalamu wa kutegua mabomu wawasili eneo la tukio ambapo watu kadhaa wanasadikiwa kupoteza maisha.