Back to top

Naibu Waziri akataa kuwasha umeme wa REA katika vijiji 3 Singida

12 October 2018
Share

Naibu Waziri wa Nishati Mheshimiwa Subira Mgalu amekataa  kuwasha umeme wa REA  katika vijiji vitatu  vya halmashauri ya singida ,kufuatia miradi hiyo kuonekana kasi yake ya kuweka nyaya ni ndogo hadi sasa ni  nyumba moja tu ndiyo iliyo unganishwa umeme kwa kipindi cha zaidi ya miezi mitano .
 
Mheshimiwa Mgalu ametoa uamuzi huo  kufuatia malalamiko ya  kucheleweshewa kuunganishiwa umeme licha ya wananchi kuweka miundombinu ya nyaya kwenye  nyumba zao.