Zimebainika changamoto kwa baadhi ya wateja wa mfuko wa taifa wa bima ya afya kwenda kuwatibu ndugu zao ambao si wanachama kupitia kadi zao na wengine wakienda kutibiwa na kadi za ndugu zao hali inayoleta mkanganyiko mteja anapofariki huku kadi aliyonayo ikisomeka jina la mtu mwingine.
Wadau wa mfuko wa taifa wa afya (NHIF) ambao ni waganga katika Zahanati,vituo vya afya na Hospitali wanaeleza changamoto wanazokumbana nazo katika kuwahudumia wateja wa naotibiwa kupitia bima ya afya ambao wana uelewa mdogo kuhusu mfuko huo
Kwa upande wake meneja wa NHIF mkoa wa Ruvuma Bw. Abdiel Mkaro anamesema mfuko huo utawachukulia hatua za kisheria wanaotibiwa kupiti kadi za ndugu zao ilhali wao si wanachama wa mfuko huo huku akieleza mkanganyiko unaojitokeza mteja anayeotibiwa kwa kadi isiyo yake anapofariki.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya mbinga Bw.Cosmas Nshenye amewataka madaktari kutoa huduma nzuri kwa wateja wa bima ya afya.