Mvua zinazoendela kunyesha wilayani Bukoba mkoani Kagera zimesababisha nyumba zaidi ya mia moja kuzingirwa na maji kufuatia mitaro inayosafirisha maji kuelekea ziwa victoria kubomoka na mingine kushindwa kupitisha maji hali inayopelekea baadhi ya wananchi kulazimika kuhama makazi yao.
.
Aidha, mkuu wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera Deodatus Kinawilo, amewataka watu waliojenga katika eneo la Nyamkazi na pembezoni mwa ziwa victoria kuchukua tahadhari ya kuhama mapema kutokana na kina cha ziwa hilo kuongezeka na kusababisha, maji kupelekwa upande wa makazi ya wananchi.