Wakulima wilayani Handeni wameiomba serikali kuwasaidia kukabiliana na panya waharibifu wanaoshambulia mazao ikiwemo muhogo na mahindi.
Hata hivyo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bwana Ramadhani Diliwa amewataka wananchi na madiwani kutoa taarifa kwa maafisa kilimo wa kata ili tatizo hilo liweze kutatuliwa.