Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Baba Mtakatifu Papa Fransisco ametuma salamu za rambirambi kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere.
Katika salamu hizo kupitia kwa Balozi wake nchini Baba Mtakatifu amewapa pole wote walioko kwenye majonzi na kuwapa moyo wanaotafuta ndugu ambao hawajapatikana.
Amemuomba Mungu awajalie baraka,nguvu na faraja wote walioguswa na msiba huo.