Back to top

Prof.Mbarawa alia wizi,uzembe,usimamizi mbovu miradi ya maji

24 January 2020
Share

Kutokana na kukithiri kwa vitendo vya wizi,uzembe na usimamizi mbovu  katika miradi mikubwa ya maji hapa nchini, waziri wa  maji Profesa Makame Mbarawa amekiagiza chuo cha maji kufundisha uzalendo, nidhamu na maadili  ili kuondoa tatizo hilo.

WaziriMbarawa amesema hayo mjini Morogoro wakati akizindua  bodi ya ushauri ya chuo cha maji ambapo akasema kumekuwepo na vitendo vingi vya hovyo vinavyofanywa na baadhi ya watendaji wa sekta ya maji hasa katika miradi inayoendelea hivyo kuisababishia serikali hasara kubwa.

Waziri huyo akatoa mifano ya wahandisi wazembe waliotaka kuisababishia serikali hasara ya mamilioni ya fedha kwenye moja ya mradi kwa kufanya upembuzi wa hovyo, kwa kulazimisha gharama kubwa ya matumizi ya bomba kubwa  la maji la chuma  wakati kukiwa na uwezekano wa kuweka bomba la plastiki.