Back to top

Rais Dkt.Magufuli afanya uteuzi wa wenyeviti watatu wa bodi.

31 January 2020
Share

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wenyeviti 3 watakaoongoza bodi za taasisi 2 za Serikali na 1 ya ubia wa Serikali na Sekta Binafsi.

Kwanza, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Gabriel Pascal Malata kuwa Mwenyekiti na Mjumbe wa kuiwakilisha Serikali katika Bodi ya Kampuni ya Airtel Tanzania Ltd.

Bw. Malata ni Naibu Wakili Mkuu wa Serikali.

Pili, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Martha Qorro kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (Institute of Rural Development Planning - IRDP).
Prof. Martha Qorro ni Profesa Mshiriki wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Tatu, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Joseph Rwegasira Buchweshaija kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa viongozi hawa umeanza tarehe 30 Januari, 2020.