Back to top

Serikali kuifanya shule aliyosoma Baba wa Taifa kuwa ya kihistoria.

07 December 2019
Share


Serikali  imesema kuwa imeamua kuifanya shule ya msingi ya Mwisenge iliyopo Musoma mkoani Mara aliyosoma Baba wa taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere  kuwa shule ya kihistoria ikiwa ni sehemu moja wapo ya kumuenzi baba wa taifa huku ikitoa zaidi ya milioni 780  kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo.

Hayo yameelezwa na Waziri mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Musona  na kutembelea shule hiyo inayoendelea kukarabatiwa.

Waziri mkuu amesema kuwa shule hiyo ya Mwisenge itaubeba mkoa wa Mara  kwa kuwa na historia ya vongozi wakubwa kupitia shuleni hapo.