Serikali imesema haijasitisha huduma wala elimu ya uzazi wa mpango bali kwa sasa wamesitisha matangazo ya uzazi wa mpango kwa muda kwenye vyombo vya habari ili kuyapitia upya na kuhakikisha maudhui yanayoifikia jamii yanakuwa na muonekano ambao serikali imekusudia.
Hayo yamezungumzwa na Naibu Waziri wa Afya Dkt.Faustine Ndungulile katika mahojiano maalum na ITV.