Back to top

Serikali yaonya shughuli za kibinadamu kwenye mapito ya wanyamapori

25 May 2020
Share

Serikali imesema itachukua hatua kali kwa watu wanaokaidi amri ya kuwataka kutokujenga na kufanya shughuli za kibinadamu kwenye mapito ya wanyamapori  (ushoroba)  kwa kuwa wanachangia kufifisha juhudi za wadau wa uhifadhi  na kusababisha migogoro inayoendelea kushamiri kati ya binadamu na wanyamapori .

Akizungumza na wadau wa uhifadhi mkoani Manyara,naibu waziri wa maliasili na utalii Constantini Kanyasu amesema kuwa wanaojenga kiholela katika maeneo ya ushoroba hawatalipwa fidia na badala ake watachukuliwa hatua.


Mkurugenzi wa wanyamapori kutoka wizara ya maliasili na utalii , Dkt.Maurusu Msuha  amesema kuwa uanishwaji ,upimaji na uwekaji wa mipaka ya maeneo ya ushoroba unapaswa kuwashirikisha wananchi ili kuepuka migogoro isiyokua ya lazima.

Katibu wa jumuiya ya hifadhi ya jamii  Burunge Bw.Benson Mwaise  na mkuu wa wilaya ya Babati Bi.Elizabeth Kitundu wamesema kuwa elimu kwa  wananchi inahitajika ili kufanikiwa kulinda ushoroba.