Back to top

Sherehe za mashujaa zaahirishwa.

18 July 2020
Share

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameahirisha sherehe za Mashujaa zilizopaswa kufanyika tarehe 25 Julai, 2020 Jijini Dodoma.

Pamoja na kuahirisha sherehe hizo, Mhe. Rais Magufuli amewataka watanzania wote kutumia siku hiyo kuwakumbuka na kuwaombea Mashujaa wote waliojitoa kwa ajili ya nchi yetu na hata wale ambao wametoa mchango mkubwa katika ngazi mbalimbali zikiwemo mtu mmojammoja na familia.

Mhe. Rais Magufuli amewatakia heri Watanzania wote kuelekea siku hiyo na amewataka kuendelea kudumisha amani, upendo, utulivu na mshikamano.