Back to top

Shule ya msingi Mandera yakabiliwa na uchakavu wa majengo.

19 April 2021
Share

Shule ya msingi Mandera iliyopo kata ya Mswaha wilayani Korogwe mkoani Tanga inakabiliwa na uchakavu mkubwa wa majengo ikiwemo vyumba vya madarasa  na nyumba za walimu hali inayo watia hofu walimu wanaofundisha katika shule hiyo.

Akizungumza na ITV Afisa elimu wa kata amesema uchakavu wa shule hiyo haukuishia kwenye vyumba vya madarasa bali hata kwenye nyumba za walimu kwani walimu hao wanalazimika kuishi wanne kwenye nyumba moja kutokana na nyumba nyingine kuezuliwa na upepo.