Back to top

Taasisi za mazingira zapambana kuokoa miti iliyo hatarini kupotea.

16 December 2018
Share

Shirika linaloshughulika na mazingira  na maendeleo (MCDI) kwa ufadhili wa shirika la mazingira duniani( WWF) linapambana kuokoa miti iliyo hatarini kupotea ukiwemo  wa  mnungunungu ambao wananchi wamekuwa wakitumia majani yake kwa tiba.

Akizungumza katika mahojiano na ITV Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo wanamazingira Afisa wa shirika la   MCDI Bw. Kassim Ulega  anasema ili kuuokoa mti huo  wameanza kuotesha miche ya mnungunungu katika kijiji cha Mchakama mkoani Lindi.