Back to top

Uhamiaji kutumia Boti za kisasa kupambana na uhamiaji haramu.

22 July 2018
Share

Kamishna wa uhamiaji nchini kamishna Generali Dkt. Anna Makakala amesema idara yake imejipanga kuweka Boti za kisasa katika mipaka inayotumia maji kutengenisha Tanzania na nchi nyingine ikiwemo ziwa Nyasa ili kukabiliana na wimbi la wahamiaji haramu.

Ameyasema hayo baada ya kutembelea kituo cha uhamiaji cha Mbamba Bay wilayani Nyasa mkoani Ruvuma na kutembelea mpaka wa Tanzania na Malawi wa ziwa Nyasa  ambapo amehitimisha  ziara yake ya siku  mbili mkoani Ruvuma.

Awali  afisa uhamiaji wa wilaya ya Nyasa mrakibu msaidizi wa uhamiaji  wa wilaya ya Nyasa Kibuga Dominick amesema kuwa  katika ziwa Nyasa wahamiaji haramu wamekuwa wakitumia ziwa Nyasa kama mlango wa kutokea kuelekea nchi mbali mbali ambapo  mwaka huu wamekamata wahamiaji haramu  15  huku wasafirishji wa wahamiaji hao wakitelekeza boti waliyotumia kusafirisha  wahamiaji na madumu mawili ya mafuta.