Back to top

Vifo kutokana na Corona Kenya vyafikia 36, walioambukizwa sasa 715.

12 May 2020
Share

Watu waliofariki kutokana na Virusi vya Corona nchini Kenya wafikia 36, Walioambukizwa 715 huku watu 259 wakiwa wamepona na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya nchini humo imeeleza kuwa Mtoto wa mwaka mmoja na miezi minane ni miongoni mwa waliotambuliwa kuwa na virusi hivyo baada ya sampuli 978 kufanyiwa vipimo katika saa 24 zilizopita.

Naibu Waziri wa Afya Dkt.Rashid Aman ameeleza kuwa raia wawili wa Tanzania ni miongoni mwa waliothibitishwa kuwa na virusi vya Corona katika kituo cha mpakani cha Isebania baada ya kupimwa na hivyo wamerejeshwa Tanzania.

Aidha wizara hiyo ya Afya imefafanua kuwa watu wawili walifariki wakiwa nyumbani na mwingine mmoja akiwa hospitalini ambao wamefikisha idadi ya waliofariki kufikia 36, huku maambukizi mapya 15 ya virusi vya Corona yaliyofanya idadi 715 ya walioambukizwa, 14 wakiwa wakenya na raia mmoja wa Rwanda.