Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Job Ndugai amewataka wabunge wa CHADEMA ambao hawashiriki vikao vya bunge kwa madai kuwa wapo karantini watambue wanachofanya ni kinyume na sheria na kuna masuala wanatakiwa kufanya ili waruhusiwe kuingia bungeni humo.
Spika Ndugai ameliambia bunge kuwa wabunge hao wanahesabika kama watoro,wanatakiwa kurejesha fedha zote walizolipwa kwa kipindi ambacho hawatakuwepo bungeni sambamba na kuwa na vipimo vikithibitisha wapo salama dhidi ya ugonjwa wa virusi vya corona.