Back to top

Wadau waanza kuchukua hatua za kunusuru uhifadhi Manyara Tarangire

23 May 2018
Share

Serikali shirika la hifadhi za taifa na wadau wa uhifadhi wameanza kuchukua hatua  za kunusuru  Ikolojia ya hifadhi ya ziwa Manyara na Tarangire kwa kuimalisha maeneo ya mapito ya wanyamapori (SHOROBA) yanayoathiriwa na shughuli za kibinadamu zinazotisha kukauka kwa ziwa Manyara na kutishia  kufunga mapito ya wanyamapori (SHOROBA) wanaokwenda na kurudi katika hifadhi za Manyara na Tarangire

Wakuu wa wilaya ya Karatu  Therecia Mahongo  anasema mpango huo unahusisha kuwaondoa watu wanaofanya shughuli za kilimo holela katika maeneo hayo na wanaoharibu mazingira kwenye mapito ya wanyamapori.

Mhifadhi mkuu wa hifadhi ya taifa ya ziwa Manyara Noelia Myonga anasema shughuli za kibindamu zinazofanywa katika  maeneo ya miinuka  katika  wilaya za Karatu na Babati  kwa kiasi kikubwa zimeathiri ziwa Manyara  ambalo ndiyo tegemeo pekee la hifadhi hiyo.

Viongozi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi  pamoja na  maeneo ya mapito ya wanyamapori wanasema wameanza kushirikiana na uongozi wa hifadhi katika kukomesha tabia hizo.