Back to top

Waendesha pikipiki Arumeru walalamikia kutekwa na kuporwa pikipiki

14 January 2020
Share

Waendesha pikipiki wilayani Arumeru  mkoani  Arusha wamelalamikia kuibuka  kwa mtandao wa  watu wanaokodisha pikipiki zao  na baadaye  kuwateka, kupora na  kuwaua jambo linalosababisha washindwe  kufanya kazi  kwa  amani  hasa  nyakati za usiku na wameomba serikali kufuatilia na kukomesha mtandao huo.

Vilio vya vijana wanaoendesha pikipiki vya kutekwa,kuporwa pikipiki na  kisha  kuuawa nyakati za usiku vimekuwa vikisikika katika maeneo  mbalimbali  nchini na licha ya  kuwepo kwa jitihada kubwa za kuvikabili tatizo  bado ni kubwa