Back to top

Wagonjwa wa Corona Kenya wafikia 50.

30 March 2020
Share

Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona nchini Kenya imeongezeka na kufikia 50,hii ni baada ya watu wengine 8 kuthibitishwa kuwa na virusi hivyo katika muda wa saa 24 zilizopita.

Maambukizi hayo mapya yakiwa ni ya Mkenya mmoja ambaye yuko karantini na wengine 7 waliochangamana na wagonjwa wa hapo awali.
]
Waziri wa afya Mutahi Kagwe anasema kuwa Nairobi inaongeza kwenye maambukizi hayo kwa wagonjwa 34,Mombasa 3,Kilifi 6,Kajiado 3,Kwale 3 na Kaunti ya kitui 1.