Back to top

Wakazi 36,000 kunufaika na huduma ya umeme wilayani Mlele.

12 September 2018
Share

Zaidi ya wakazi elfu thelathini na sita wa kata ya Majimoto katika halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoani Katavi  watanufaika na huduma ya nishati ya umeme ikiwemo  kuondokana na adha ya kutumia tochi katika zahanati  baada ya  mradi wa kusambaza nishati ya umeme vijijini (REA) awamu ya tatu kuanza kutekelezwa mkoani humo.

Akizungumza na wananchi wa kata ya Majimoto waziri wa nishati Dkt. Medard Kalemani amesema mradi huo kwa awamu hii  utaunganisha umeme katika taasisi zote za umma ,vijiji vyote na vitongoji vyake

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mlele Bi.Rachel Kasanda amesema wilaya ina jumla ya viwanda 236 ambapo  30 kati ya hivyo ni viwanda vya kati huku asilimia 60 vikiwa   katika kata ya majimoto

Mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka miwili unatarajiwa kukamilika mwezi juni mwaka 2020.