Serikali imetoa wito kwa wakulima kutumia bima za mazao ili kuepuka hasara na athari zinazotokana na majanga mbalimbali ikiwemo mafuriko pamoja na ukame.
.
Wito huo umetolewa Jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya baada ya majadiliano na wadau wa maendeleo kutoka nchini Japan na serikali ya Tanzania.