Back to top

Walioambukizwa Corona Uganda wafikia 18.

27 March 2020
Share

Idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa homa ya Corona nchini Uganda yafikia 18.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni kupitia kwenye mitandao yake ya kijamii ameandika kwamba watu wengine 4 wameambukizwa na kirusi cha Corona na kufanya idadi ya wagonjwa kufikia 18.

Museveni amesema watu hao 4 ni miongoni mwa raia waliosafiri kutoka Dubai na kuwekwa karatini.