Wanafunzi 13 wa shule ya msingi ya Kakamega nchini Kenya wamefariki dunia na wengine 39 kujeruhiwa baada ya kukanyagana kwenye ngazi ya kushukia kutoka darasani,baada ya kengele ya kumaliza masomo kugongwa.
Kamanda wa polisi Ukanda wa Magharibi mwa Kenya Peris Kimani amesema tukio hilo limetokea wanafunzi walipokuwa wakielekea nyumbani baada ya kukamilika kwa vipindi jioni ya leo.
Kamanda Kimani amethibitisha kuwa wanafunzi 20 wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani.