Baadhi ya wananchi wanaoishi katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, wamewataka wenzao kuacha tabia ya kuchagua kazi za kufanya na badala yake wajiingize katika ujasiriamali na kzualisha bidhaa mbalimbali zinazotumiwa kwa wingi katika jamii ikiwemo majiko ya mkaa ,karai za kukaangia chips na vifaa vingine vya matumizi ya jikoni.
"kama mtu haujasoma hauwezi kuchagua kazi ya kufanyaj, inayokuja mbele yako ndio utakayoifanya ili kuweza kuendesha maisha yako ya kila siku na familia kwa ujumla".anasema Issa abadani - mkazi manispaa ya Lindi