Wananchi wa vijiji vya Amka na Nandembo katika wilaya ya Tunduru mkoa wa Ruvuma, wanaeleza kukumbwa na shida kubwa ya maji na kuiomba serikali kuwachukulia hatua waliojenga mradi wa maji chini ya kiwango ambao uligharimu zaidi ya shilingi milioni 300 lakini haujawahi kutoa maji tangu mwaka 2012 ulipokabidhiwa.