Wanariadha watanzania wameng’ara katika Nagai Marathon huku wanariadha wake wakiongoza katika full marathon na half marathon
Katika full marathon kwa wanaume Marco Joseph amemaliza Nafasi ya kwanza akitumia saa 02 :21:13 huku mtanzania mwingine Willbaldo Peter akimaliza nafasi ya pili na kwa wanawake Angel John ameshika nafasi ya kwanza akitumia muda wa 02:43:21
Katika half marathon mwanariadha mzoefu Fabian Joseph amemaliza Nafasi ya kwanza akitumia saa 01:02:53 na kwa wanawake Amina Mohamedi akimaliza wa kwanza akitumia muda wa saa 01:16:08 huku watanzani wengine wakishika nafasi ya pili mpaka ya tano