Back to top

Watu wanne wamepoteza maisha katika ajali Ubungo.

12 June 2018
Share

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimethibitisha kupoteza watu wanne kati ya watano waliohusika kwenye ajali ya gari la wagonjwa kugongwa na lori eneo la Riverside Ubungo jijini Dar es salaam jana usiku.

Taarifa ya Makamu Mkuu wa Chuo hicho  prof. William Anangisye kwa vyombo vya habari imesema ajali hiyo imetokea wakati  gari la wagonjwa wa chuo likiwakimbiza  wanafunzi wawili  kutoka zahanati ya  Mabibo  kwenda kituo cha afya cha Chuo kikuu kwa matibabu zaidi.

Waliopoteza maisha ni pamoja na dereva mwandamizi wa gari la wagonjwa  James Josephat, muuguzi msaidizi Jonathan Bashuda,mwanafunzi wa  mwaka wa pili  Erasto  Sango na  mwanafunzi wa mwaka wa kwanza  Mary Godian.
Mwanafunzi mwingine  Nkiko Abishai wa mwaka wa tatu  alijeruhiwa  na kulazwa  hospitali ya  Muhimbili  akiendelea kupokea matibabu.

Mwenyezi mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi amina.