Watu wawili wamefariki dunia katika kata ya Matumbi halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma kwa kusombwa na maji ya mto huku baadhi ya barabara na madaraja yakiathirika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Diwani wa kata ya Matumbi Bw.Valentine Mtemauti amesema mito kwenye kata yake imefurika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha ambapo mkazi wa kata hiyo Shomari Saidi amesombwa na maji ya mto Luhuji na kupoteza maisha huku barabara ya Madaba-Ifinga ikiharibika na kukaribia kukatika
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi.Christina Mndeme amewataka wananchi kuchukua tahadhari kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.